31 August, 2012

RUNGU LA YESU: HARAKATI ZIMEPAMBA MOTO

Mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania George Aidan Rungu maarufu kama Rungu La Yesu hivi karibuni amekua moto wa kuotea mbali katika kupeleka mbele mziki wa injili,Rungu la Yesu ambaye anafanya mziki wa injili wa injili kwa mahadhi ya kufoka foka au gospel hiphop  kama wanavyoita amekua akifanya harakati hizi kwa muda mrefu lakini kwa kipindi hiki anaonekana kuongeza cheche vilivyo,wiki mbilii zilizopita Rungu la Yesu  alikua mmoja kati ya wahusika wakuu wa uandaaji wa tamasha la Ze sunday Of Gospel Hiphop tamasha ambalo lilionekana kuwabariki watu wengii wanaopenda mziki wa aina hiyo,tulipoongea nae Rungu la Yesu Alikua na haya ya kusema,"Nachoweza kusema ni kwamba harakati zimepamba moto,unajua harakati zilikwepo toka kitambo ila kilichofanyika sasa ni utanuzi wa wigo wa harakati na huduma,kama unavyojua siku hizi kuna wigo mpana sana katika mitandao ya jamii kutumika kufanyia harakati na ndo mana watu wanaweza kuona harakati zetu kwa urahisi tofauti na zamani kabla ya vitu hivi kuwepo,kuhusu tamasha ni kweli tuliandaa tamasha tarehe 19 ambao waandaji wakuu tulikuaa  ni ZE GCRZ,ZE God'z Chosen Rapperz familia ya mziki ambayo inatujumisha member saba lakini kwa ajilii ya majukumu mkoani dar es alaam tumebaki member watatu ambao ni  mimi mwenyewe Rungu la Yesu,Sir.Mbezi junior ambae ndiye founder na Preacher Gazuko,wengine ambao wako mikoani ni Dialo Antony ambae kwa sasa ki makazi yupo Arusha,Eriki kapinga yuko Songea,Eka injili yuko masomoni mbeya,Stani boi,na Ben Mayige ambaye kama akikubali atakua member rasmi wa Ze GCRZ,harakati hazijaishia hapo,  kwa sababu bado tunapanga ratiba za harakati ambapo jumapili ya kwanza ya mwezi wa kumi tunatarajia kuwepo na tamasha kubwa pia,tumeweka mbali kidogo ili tuweze ku cope na personal timetable za kila mtu mfano binafsi nina tour nyingi katikati hapa tuna mkutano wainjili tabora mwezi wa tisa,baada ya hapo nitaelekea Tanga kisha ntarudi Dar kwa ajili ya tamasha baada ya hapo nitakua najiandaa na mkutano mwingine pande za mbinga"pia Rungu alifunguka kuhusu project yake mpya,"kwa sasa hivi siwezi kuiongelea sana mpaka pale itakapokua tayari ila kwa ufupi namalizia project yangu ya album pale combimation sounds chini ya man walter ambayo kama haitabadilika nitaipa jina la Ulokole sio fasheni,kwa sasa nmerelease track inayoitwa Bwana Yesu asifiwe ambayo pia nimeifanya kwa man walter".Rungu alikua na hawa wakuwashukuru,"Namshukuru sana Mungu kwa kunipa kibali katika ulimwengu wa sasa,naishukuru familia yangu,ZE GCRZ kwa kuwa nami katika harakati,nawashukuru wana gospel hiphop wote ni wengi kuwataja na kwa upekee nampenda kumshukuru ma bro George Maige kwa kuni support bila kuwasahau nyie wana habari Mungu awabariki"hivyo ndivyo Rungu la Yesu alivyofunguka kwa habari zaidi kuhusu yeye na nyingine nezo nyingi endelea kuwa nasi..

No comments:

Post a Comment